Kiswahili sanifu kidato cha sita

 

Kitabu hiki kinaundwa na sura nne ambazo ni: FASIHI, MYAMBULIKO WA VITENZI,
UAMBISHAJI WA VITENZI NA MANENO YA KISWAHILI, UTUNGAJI (Risala na
hotuba). Mwishoni mwa kila sura kumeandaliwa mazoezi ambayo yatawasaidia
wanafunzi kufungua akili na kujaribu kuzama katika mada zilizojadiliwa kitabuni.
Katika kitabu hiki mkazo ni kueleza maana ya mnyambuliko na uambishaji wa vitenzi
kama sehemu moja ya sarufi ambayo haikujadiliwa zaidi katika vitabu vilivyotangulia.
Somo hili litamwongezea mwanafunzi ustadi wa lugha hii ya Kiswahili.
Uandishi wenyewe wa kitabu ulifanywa na NDAYAMBAJE Ladislas na NIYIRORA
Emmanuel kutoka Chuo Kikuu cha Elimu cha Kigali (KIE).